Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

MADALALI WA MINADA KUSAJILIWA KIELEKTRONIKI

12 Aug, 2022
MADALALI WA MINADA KUSAJILIWA KIELEKTRONIKI

Wizara ya Fedha na Mipango imeandaa mfumo wa kielektroniki wa utoaji Leseni za Udalali na Uendeshaji minada ya hadhara ambao utawezesha uombaji na upatikanaji wa Leseni kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia simu za mkononi ili kuwaondolea wananchi adha na gharama ya kufuata leseni hizo Makao Makuu - Dodoma.

Akizungumza wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea banda la Wizara katika Maonesho ya Nanenane jijini Mbeya, Msimamizi wa mali za Serikali wizarani hapo, Bw. George Killo, alisema kuwa mfumo huo utamuwezesha mwananchi kufanya usajili popote alipo hivyo kupata leseni yake kwa wakati.

‘Mwombaji wa leseni ya udalali anapaswa kujisajili kupitia tovuti ya Wizara (www.mof.go.tz) na kisha kubonyeza kipengele cha GAMIS na kujisajili, kujaza taarifa zinazohitajika, kujaza fomu za maombi kikamilifu na kuwasilisha kwa Katibu Tawala wa Wilaya husika kwa ajili ya uhakiki na saini.’ Alieleza Bw. Killo.

Alisema mwombaji wa Leseni za Udalali na Uendeshaji Minada ya hadhara anahitajika kuwa na fumu ya maombi iliyojazwa kikamilifu na kugongwa mhuri na Katibu Tawala wa Wilaya husika, Tax Clearance Certificate/incorporation, leseni ya biashara pamoja na Tax Clearance Certificate na viambatisho hivyo viwe katika mfumo wa PDF.

Alisema kupitia mfumo huo mwombaji anaweza kupata taarifa za maombi yake ikiwa yametumwa, yamekataliwa au yamekamilika na waombaji waliofanikiwa wataorodheshwa Katika tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango na kuchukua leseni zao katika Ofisi ya Usimamizi wa Mali za Serikali katika mikoa yao. 

Bw. Killo alifafanua kuwa Leseni hizo zinatumika katika uendeshaji wa minada ya hadhara, ukusanyaji wa madeni, ushuru, tozo, udalali wa mahakama, udalali wa nyumba na viwanja na hutolewa kwa muda wa mwaka (Januari -Disemba) kwa Sh. 150,000/= na nusu mwaka (Januari – June) (Julai – Disemba) kwa Sh.75,000.

Alisema dalali yoyote ambaye anaendesha mnada wa hadhara anatakiwa awe amesajiliwa na awe na leseni ya halali ambayo haijaisha muda wake wa matumizi inayotolewa na Wizara yetu ya Fedha na Mipango.

Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zilizochini yake inashiriki katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa jijini Mbeya yenye kauli mbiu ‘Ajenda 10/30- Kilimo ni biashara, shiriki kuhesabiwa kwa mipango bora ya Kilimo, Uvuvi Na Mifugo”.

Mwisho.