Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

WIZARA YA FEDHA YAENDELEA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.

14 Aug, 2024
WIZARA YA FEDHA YAENDELEA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.
Afisa Ushirika kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC), Bw. Adolf Ndunguru, akigawa vipeperushi vyenye mada mbalimbali ikiwemo mikopo, akiba uwekezaji kwa baadhi ya wananchi wa Wilaya vya Mtama mkoani Lindi, waliojitokeza kupata elimu ya masuala ya fedha.
 
Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na wadau wa Sekta ya Fedha nchini, inaendelea na zoezi la utoaji elimu ya fedha kwa wananchi wa makundi mbalimbali ikiwemo Wahamasishaji wa Biashara ya Huduma Ndogo za Fedha, Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo, Vikundi vya Kijamii vya Huduma Ndogo za Fedha, Watoa Huduma za Fedha, Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Mahitaji Maalum.
 
Lengo la kutoa elimu hiyo  ni kuhakikisha inaongeza idadi  kubwa ya watu wenye uelewa mpana wa  masuala ya fedha na kupata maarifa juu ya upatikanaji na utumiaji wa huduma rasmi za kifedha.
 
Wizara ya Fedha inaendelea kuwasisitiza Wananchi kutoa taarifa kwa Mamlaka husika pindi wanapobaini kuwepo wa Mtoa Huduma asiyesajiliwa au anayetoa huduma za fedha hizo kinyume cha Sheria na utaratibu uliowekwa na Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
 
MWISHO.