Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

SWEDEN YAAHIDI KUSAIDIA UJENZI WA RELI YA KISASA SGR

22 Mar, 2024
SWEDEN YAAHIDI KUSAIDIA UJENZI WA RELI YA KISASA SGR
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akimkabidhi zawadi Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na Biashara ya Nje wa Sweden Mhe. Diana Janse, baada ya kumaliza kikao kilichojadili kuhusu ushirikiano kati ya nchi hizo mbili na utekelezaji wa miradi ikiwemo elimu, usawa wa kijinsia, mazingira na masuala ya miundombinu hususan reli ya SGR kilichofanyika jijini Dodoma.
 
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa na Biashara ya Nje wa Sweden, Mhe. Diana Janse, jijini Dodoma, ambapo Naibu Waziri huyo, amemweleza Mhe. Dkt. Nchemba kuwa, nchi yake inaandaa Mkakati Mpya wa Ushirikiano kati ya nchi hizo mbili unaolenga kuongeza ushirikiano katika Nyanja za kiuchumi na kibiashara.
 
Katika mazungumzo yao, Mhe. Dkt. Nchemba aliishukuru Sweden kwa kusaidia maendeleo ya nchi kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa katika sekta za nishati, elimu, maendeleo ya Jamii kupitia Mfuko wa TASAF pamoja na mradi wa ujenzi wa reli ya Kisasa SGR, kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Singida ambacho ujenzi wake umekamilika kwa zaidi ya asilimia 96.
 
Aidha, Dkt. Nchemba ameishukuru Sweden kwa kuonesha nia ya kutoa zaidi ya dola za Marekani milioni 580 kwa ajili ya ujenzi wa kipande cha tatu na cha nne cha reli ya kisasa SGR, fedha ambazo nchi hiyo itazitoa hivi karibuni baada ya kukamilika kwa tathimini ya mazingira ya mradi huo.
 
Kuhusu Mkakati Mpya wa Ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Nchemba aliahidi kuwa Tanzania itashiriki kikamilifu katika kufanikisha mkakati huo na kuwakaribisha wawekezaji kutoka Sweden kuja kuwekeza mitaji na teknolojia hapa nchini ili kuchochea akuaji wa uchumi, ajira na maendeleo ya nchi kwa ujumla.
 
Naibu Waziri huyo wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa, Mhe. Diana Jense, alisema kuwa nchi yake inatambua kuwa mradi wa Reli ya Kisasa ni moja ya miradi ya kipaumbele kwa Tanzania na kwamba nchi yake iko tayari kushiriki katika ujenzi wa mradi huo.
 
Alisema pia kuwa mwelekeo mpya wa ushirikiano wa kimataifa kati ya Tanzania na Sweden utajielekeza zaidi katika masuala ya kiuchumi na kibiashara ambapo utalenga zaidi kuvutia uwekezaji kupitia sekta binafsi.
 
Aidha, katika mkutano huo uliohudhuriwa pia na Balozi wa Sweden Nchini Tanzania, Mhe. Charlotta Ozaki Macias na naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Chriastian Omolo, Viongozi hao walijadili kuhusu uwekezaji katika mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam ambapo nchi hiyo inataka kuwekeza kupitia kampuni ya Scania, hatua inayolenga kupunguza changamoto ya usafiri katika jiji hilo la kibiashara.
 
Mwisho.