Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

SERIKALI HAINA KESI ZA KODI ZA SH. TRILIONI 360

23 Sep, 2022
SERIKALI HAINA KESI ZA KODI ZA SH. TRILIONI 360

Serikali imesema kuwa haina kesi 1,097 za kodi za muda mrefu zenye thamani ya Sh. trilioni 360 na dola za Marekani milioni 181.4 ambazo hazijaamuliwa katika Bodi ya Rufaa za Kodi (TRAB) na Baraza la Rufaa la Kodi (TRAT) bali kuna mashauri 854 yaliyo kwenye hatua mbalimbali za usikilizaji, yenye kodi inayobishaniwa ya jumla ya Sh. trilioni 4.21 na dola za Marekani milioni 3.48.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dk. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kisesa, Mhe. Luhaga Joelson Mpina, aliyetaka kujua sababu inayofanya kesi 1,097 za kodi za muda mrefu zenye thamani ya Shilingi trilioni 360 na dola za Marekani milioni 181.4 hazijaamuliwa hadi sasa.

Akifafanua kuhusu kiasi cha Sh. bilioni 700 kilichopokelewa na Serikali Mhe. Nchemba alisema kuwa kiasi hicho kilikuwa sehemu ya makubaliano yaliyofikiwa baada ya kuundwa timu ya kusimamia makubaliano hayo mwaka 2017/2018 kati ya Serikali na Kampuni ya Barick.

‘‘Makubaliano hayo yaliisha Januari 24, 2020 ambapo Tanzania ilikubali kuachilia Sh. trilioni 360 ili kumaliza shauri lile na kuunda Kampuni ya Twiga ambapo Serikali ina ubia asilimia 16 na Kampuni ya Baricki ina asilimia 84’’, alisema Mhe. Nchemba.

Alisema makubaliano hayo pia yaliifanya Kampuni ya Barick kufuta kesi iliyofungua dhidi ya Tanzania iliyokuwa na madai ya dola za Marekani bilioni 2.7 na kukubaliana Kampuni hiyo itoe dola za Marekani milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na pia kutoa dola 6 kwenye kila dhahabu na dola za Marekani milioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa maabara ya madini.

Aidha, Mhe. Nchemba ameeleza kuwa kwa sasa taasisi za rufaa za kodi zinaendelea kusikiliza mashauri hayo pamoja na mashauri mapya yanayoendelea kusajiliwa kwani idadi ya mashauri ya kodi hupungua au kuongezeka kulingana na kasi ya usikilizaji na usajili kwa nyakati tofauti.

Mwisho.