Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

OFISI YA TRA MBULU KUJENGWA 2026/27

28 May, 2025
OFISI YA TRA MBULU KUJENGWA 2026/27

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akijibu swali la  Mbunge wa Mbulu Mjini, Mhe. Zacharia Paulo Issaay, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Mbulu, jijini Dodoma.

 

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amesema kuwa Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ina mpango wa kuanza ujenzi wa Ofisi ya TRA katika Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara, katika mwaka 2026/27. 

Aliyasema hayo bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbulu Mjini, Mhe. Zacharia Paulo Issaay, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Ofisi ya TRA katika Wilaya hiyo.

Alifafanua kuwa katika kipindi ambacho hakuna Ofisi ya TRA, shughuli za ukusanyaji wa mapato ya Serikali zinafanyika kwenye jengo la iliyokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

MWISHO.