Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

DKT. MWAMBA ATETA NA MKURUGENZI ESRF

03 Jul, 2025
DKT. MWAMBA ATETA NA MKURUGENZI ESRF

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (wa nne kulia) na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Prof. Fortunata Makene (wa nne kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Wizara ya Fedha na Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESFR), baada ya kikao kilichofanyika ofisini kwake, Treasury Square, jijini Dodoma.

 

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Prof. Fortunata Makene, kuhusu ushirikiano kati ya Serikali na Taasisi hiyo katika maendeleo ya nchi hususan katika masuala ya kiuchumi na kijamii. 

Amekutana naye ofisini kwake jijini Dodoma, ambapo alimwelezea maeneo ya kipaumbele nchini yanaongozwa kwa muda mrefu na Dira ya Maendeleo ya Taifa, kwa muda wa kati kupitia Mipango ya Maendeleo ya Miaka Mitano, na kwa muda mfupi kupitia Mpango wa Maendeleo wa kila Mwaka.

Miongoni mwa vipaumbele hivyo ni kuongeza nafasi za ajira, kupunguza kwa kiasi kikubwa viwango vya umaskini, na kuongeza mauzo ya nje na hivyo kuchangia kuchochea maendeleo jamii na nchi kwa ujumla.

MWISHO.