WATUMISHI WIZARA YA FEDHA WAHIMIZWA KUENDELEA KUCHAPA KAZI
Watumishi wa Wizara ya Fedha wameagizwa kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa mapato na kuratibu upatikanaji wa fedha ili kutoa fedha kwa wakati kwa ajili ya kutekeleza miradi yote iliyoidhinishwa na Bunge.
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Fedha kwa niaba ya Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakati akifungua kikao cha watumishi na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma.