WAKAZI WA BIHARAMULO KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI WA DOLA MIL.55.1 KUTOKA HUNGARY
Serikali ya Tanzania na Hungary zimesaini mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 55.1 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Biharamulo Mkoani Kagera.
Mkataba huo umesainiwa jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania akishuhudiwa na Balozi Mteule wa Hungary nchini, Mhe. Katalin Nyirati.
