WAFANYABIASHARA WATAKIWA KUSHIRIKI ZABUNI KUPITIA NeST
Serikali imewataka wafanyabiashara wazawa kujiunga na Mfumo Mpya wa Kielektroniki wa Ununuzi ya Umma (NeST) ili kupata Zabuni zinazotolewa na Serikali na kunufaika kwa kukuza pato la mtu mmoja na Taifa kwa ujumla.
Hayo yameelezwa na Kamishna wa Idara ya Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Bw. William Mhoja, wakati wa Kongamano la ukusanyaji maoni ya Kodi Kikanda Mkoani Mtwara, ikiwa ni muendelezo wa makongamano kama hayo yanayofanyika Kanda mbalimbali nchini kwa lengo la kuboresha Sera ya Kodi kwa mwaka 2024/25.