UHUSIANO WA TANZANIA NA KOREA KUSINI WAZIDI KUIMARIKA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, amesema kuwa Serikali ya Tanzania inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa Korea Kusini katika sekta mbalimbali, kupitia nafasi yake kama mshirika wa maendeleo na rafiki wa karibu.
Dkt. Mwamba amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania, Mhe. Eunje Ahn, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jjini Dar es Salaam, ambapo mazungumzo hayo yalihusu namna ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa maendeleo kati ya mataifa hayo mawili.
