TIMU YA WASHAURI KUTOKA AfDB YAVUTIWA NA UKUAJI WA UCHUMI
Washauri Waandamizi wa Wakurugenzi Watendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) wameanza ziara ya siku tano nchini kwa ajili ya kuelewa vipaumbele vya maendeleo ya Tanzania na namna AfDB inavyoweza kuchangia shughuli zenye matokeo chanya na kubadilisha maisha ya watanzania.
Akizungumza kuhusu ziara hiyo, baada ya kukutana na ujuembe huo jijini Dodoma, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, alisema kuwa ziara ya Washauri hao ni sehemu ya ajenda ya kila mwaka ya Bodi ya Wakurugenzi Watendaji wa AfDB katika nchi wanachama wa Kanda.