TIB YAAGIZWA KUHAKIKISHA INACHAGIZA UKUAJI WA MAENDELEO YA UCHUMI WA TAIFA
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameiagiza Benki ya Maendeleo ya TIB kuimarisha zaidi mifumo yake ya uendeshaji ili iweze kufikia malengo yake ya kuisaidia Serikali kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika maeneo ya kukuza uchumi wa Taifa na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.
Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ametoa maelekezo hayo Jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Benki ya Maendeleo Tanzania (TIB) ukiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Bw. Sosthenes Kewe, kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali yanayohusu kuimarisha utendaji wa benki hiyo na mchango wake katika kukuza uchumi wa Taifa.
