TANZANIA NA EXIM BANK YA MAREKANI KUENDELEZA USHIRIKIANO
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amesema kuwa ushirikiano wa Tanzania na Benki ya Exim ya Marekani, utachochea ukuaji wa uchumi wa Taifa kupitia miradi mbalimbali ya uzalishaji ikiwemo ujenzi wa miundombinu, sekta muhimu za madini, nishati, usafiri na usafirishaji na mizigo, dawa na usindikaji wa mazao ya kilimo.
Mhe. Balozi Omar alisema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Benki ya Exim ya Marekani, Bw. John Jovanovic, Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Washington D.C nchini Marekani, pembezomi mwa Mikutano ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimafaifa-IMF.
