TANZANIA NA BENKI YA ASIA (AIIB) KUSHIRIKIANA KIMKAKATI
Tanzania imeendelea kuimarisha ushirikiano wake na Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), hatua inayotarajiwa kufungua fursa mpya za ufadhili kwa miradi ya kimkakati ya maendeleo, ikiwemo maji, nishati, usafiri, teknolojia ya habari na Mawasiliano pamoja na miundombinu ya kijani.
Hayo yamejiri wakati Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alipo ongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao na Rais wa Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), Bi. Zou Jiayi, pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, jijini Washington D.C, nchini Marekani.
