TAASISI YA ATIDI YASISITIZWA KUSAIDIA SEKTA BINAFSI KUELEKEA DIRA 2050
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) ametoa rai kwa Taasisi ya Bima ya Maendeleo ya Biashara na Uwekezaji Afrika (ATIDI) kushirikiana na Tanzania hususani katika kukuza Sekta binafsi ili nchi iweze kufikia malengo ya Dira ya Taifa 2050.
Rai hiyo ameitoa wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Taasisi ya ATIDI ukiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi hiyo, Prof. Kelly Kingsly, yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma
