SERIKALI YATOA MIKOPO YA SH. BILIONI 165 KWA WAKULIMA
Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa mkopo wa shillingi billioni 164.9 kwa Sekta ya Benki na Taasisi za Fedha nchini uliowanufausha wakulima wadogo 5,385 na Vyama vya Ushirika na Masoko (AMCOS) 21.
Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Halima Mdee aliyetaka kujua makundi yaliyonufaika na mkopo wa shilingi trilioni moja iliyoahidiwa kutolewa na Serikali katika sekta ya kilimo pamoja na masharti yake.