SERIKALI NA BENKI YA DUNIA WAJADILI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO INAYOFADHILIWA NA BENKI YA DUNIA
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, ameihakikishia Benki ya Dunia kwamba, Serikali itaendelea kushirikiana na Benki hiyo katika kutekeleza miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Benki hiyo kwa ufanisi, wakati na kwa viwango vinavyokusudiwa.
Dkt. Mwamba amesema hayo wakati wa kikao cha Country Portfolio Performance Review (CPPR) kinacholenga kubaini changamoto kuu za mfumo zinazokwamisha utekelezaji wa miradi na kuandaa mpango kazi wa pamoja wa kuzitatua kilichofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.