RAIS SAMIA AHIMIZA AMANI NA UTULIVU NCHINI: ACHANGIA KANISA MILIONI 50
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa madhehebu ya dini nchini kuendelea kuliombea Taifa ili kudumisha amani na utulivu uliopo pamoja na kutekeleza mipango yao ya maendeleo inayolenga kuihudumia jamii kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 iliyozinduliwa hivi karibuni.
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa wito huo katika Hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), alipomwakilisha katika Uzinduzi wa Harambee ya Ujenzi wa Ofisi Kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Dodoma, iliyofanyika katika eneo la mradi-Nzuguni C, Jijini Dodoma.