NAIBU KATIBU MKUU JENIFA OMOLO ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA FEDHA SABASABA 2024
Wananchi wametakiwa kulipa kodi kwa hiari kwa kutambua kuwa Serikali haiwezi kutekeleza miradi ya maendeleo bila kukusanya mapato kutoka kwenye vyanzo mbalimbali zikiwemo shughuli za kila siku za mtu mmoja mmoja.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Huduma za Hazina Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo, alipotembelea Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam.