MFUMO WA GePG WAONGEZA USALAMA WA MAPATO VYUONI
Usalama wa makusanyo ya mapato ya Vyuo Vikuu na vya Kati umeongezeka kwa kiwango kikubwa baada ya kuanza kutumika kwa mfumo wa Kielektroniki wa ukusanyaji wa Mapato ya Serikali (GePG).
Hayo yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Chuo (taaluma) kutoka Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA), Dkt. Momole Kasambala, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Ubunifu yanayofanyika kitaifa katika uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma.