KATIBU MKUU HAZINA ATETA NA BALOZI WA DENMARK NCHINI TANZANIA
Denmark imeahidi kuendeleza ushirikiano zaidi na Tanzania katika jitihada zake za kuimarisha uchumi na maendeleo ya wananchi kwa kutoa fedha na misaada ya kiufundi katika sekta ya mbalimbali ikiwemo afya.
Ahadi hiyo imetolewa na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Mette Norgaard Dissingspandet alipokutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Natu El-Maamary Mwamba, katika Ofisi Ndogo za Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam.