KAMISAA MAKINDA AWATAKA WANANCHI KUTUMIA TAKWIMU SAHIHI KWA MAENDELEO
Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, ametoa rai kwa wananchi kuanzia ngazi ya chini kutumia takwimu sahihi zilizopatikana kutokana na Sensa iliyofanyika katika shughuli mbalimbali za Maendeleo.
Mhe. Makinda ametoa rai hiyo alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam, ambapo amesisitiza matumizi ya Takwimu sahihi kwa maendeleo.