IMF YAFANYA MAJADILIANO NA TANZANIA KUHUSU USHIRIKIANO WA MAENDELEO
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amefungua vikao vya majadiliano kati ya Serikali na Timu ya Wataalam kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) waliowasili nchini kwa ajili ya kufanya tathimini ili Tanzania iweze kupata fedha za awamu ya nne kupitia program ya Extended Credit Facility-(ECF), itakayowezesha kuendelea kuchachua na kuimarisha uchumi kupitia sekta za uzalishaji.
Kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma kimehusisha timu ya wataalamu kutoka IMF walioongozwa na Bw. Harris Charalambos Tsangarides waliokuja kufanya tathmini na pia kujadili namna ya kuiwezesha Tanzania kupata fedha ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kupitia dirisha lake la Resilient and Sustainable Trust (RST).