GOLDEN WOMEN WASHAURIWA KUENDELEA KUWAFIKIA WAHITAJI
Umoja wa Wanawake wa Wizara ya Fedha, (Golden Women), wameshauriwa kuendeleza utamaduni wa kutoa misaada mbalimbali kwa watu wenye mahitaji maalumu ili kuwasaidia kufikia malengo yao.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi Jenifa Christian Omolo, ametoa ushauri huo alipotembelea Kituo cha Huduma cha SAFAAD, kilichopo Kijiji cha Membe, Wilayani Chamwino mkoani Dodoma.