DKT. NCHEMBA AKUTANA NA UJUMBE WA CITIBANK KUJADILI USHIRIKIANO

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwingulu Lameck Nchemba, amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka CITI Bank Unaosimamia Ukanda wa Jangwa la Sahara na Mashariki ya Kati , ambapo benki hiyo imeahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika uendelezaji wa miradi ya maendeleo, uwekezaji na kufanya tathimini ya uwezo wa`nchi kukopesheka (credit rating).