DKT. NCHEMBA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA RAIS WA BENKI YA DUNIA JIJINI WASHINGTON
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Benki ya Dunia, Bw. David Malpass, na kujadiliana masuala kadhaa ya ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo, yatakayoiwezesha nchi kupiga hatua zaidi kimaendeleo.