DKT. NCHEMBA AITAKA IAA KUSIMAMIA KWA WELEDI UJENZI WA KAMPASI YAKE JIJINI DODOMA

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb) (kushoto), akikata utepe katika hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Jengo la Taaluma la Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) Kampasi ya Dodoma, katika eneo la Njedengwa, jijini Dodoma. Jengo hilo la ghorofa Sita lenye ukubwa wa takribani Sqm 6600, litakuwa na uwezo wa kukalisha wanafunzi 4,500 kwa wakati mmoja. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho, Dkt. Mwamini Tulli, Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Eliamani Sedoyeka na Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Mrisho Gambo.