DKT. MWAMBA: TUMIENI JUKWAA LA WANAWAKE NA KODI KUTOA ELIMU
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, amewapongeza wanawake wanaofanya kazi katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa mchango wao mkubwa katika kusimamia na kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali, akisisitiza kuwa mapato hayo ndiyo msingi wa utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Taifa.
Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, Dkt. Natu Mwamba alisema kuwa wanawake wameendelea kuwa na nafasi muhimu katika utumishi wa umma na katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.
