WIZARA YA FEDHA YASHAURIWA KUWA NA MPANGO ENDELEVU WA UTOAJI ELIMU YA FEDHA
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge, mkoani Tabora, Bw. Seleman Mohamed Pandawe, ameishauri Wizara ya Fedha kuwa na mpango endelevu na wa muda mrefu wa utoaji elimu ya fedha kwa wananchi kwa kuwa elimu hiyo ni muhimu na ina mchango katika ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
Bw. Pandawe, ametoa ushauri huo alipokutana na Timu ya Wataalamu ya Wizara ya Fedha ambayo ilifika Wilayani mwake kutoa elimu ya fedha kwa Wananchi ili waweze kutumia fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya fedha na kujikomboa kiuchumi.