WIZARA YA FEDHA YARAHISISHA UPATIKANAJI WA TAARIFA ZAKE
Wananchi wametakiwa kutumia taarifa zinazotolewa na Wizara ya Fedha kupitia njia mbalimbali za mawasiliano ili kupata taarifa mbalimbali za uchumi na fedha kwa lengo la kuawasidia kupata ufahamu na maarifa katika kukabiliana na changamoto za kiuchimi.
Hayo yamesemwa na Afisa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha, Bi. Eva Varelian, alipokuwa akitoa elimu ya taarifa za uchumi, Sera, fedha na programu za Wizara, kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha kwenye Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Dar Es salaam (Sabasaba) ambayo yameanza tarehe 28 Juni na kutarajiwa kuhitimishwa Julai 13 mwaka huu.