WIKI YA HUDUMA ZA FEDHA KUFUNGUA FURSA ZA UCHUMI
Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Wasimamzi wa Sekta ya Fedha nchini, imeandaa Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa jijini Mbeya ili kuwawezesha wananchi kupata uelewa wa masuala ya fedha.
Maadhimisho hayo yanayofanyika katika Viwanja vya Ruanda-nzovwe Jijini Mbeya yanalenga kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu matumizi ya huduma rasmi za fedha kwakuwa Serikali inakusudia takriban asilimia 80 ya wananchi watakuwa wamepata uelewa wa masuala ya fedha ifikapo mwaka 2025.