WAZIRI WA FEDHA MHE. BALOZI OMAR ATETA NA UONGOZI WA AfDB
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Kanda ya Afrika, ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Kanda ya Afrika, Bw. Ronald Cafrine, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar Es Salaam.
Katika kikao hicho Mhe. Balozi Mussa Omar pamoja na Ujumbe huo wa Benki ya AfDB, walijadili masuala mbalimbali yanayolenga kuifanya nchi ya Tanzania kufikia malengo yaliyowekwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
