WAZIRI WA FEDHA AKUTANA NA UJUMBE WA KITENGO CHA KUDHIBITI FEDHA HARAMU (FIU)
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU) ukiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Wataalamu wa Kuzuia Utakasishaji Fedha Haramu ambaye pia ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bi. Sauda Msemo, pamoja na Kamishna wa FIU, Bw. Majaba Magana.
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ya Waziri wa Fedha, jijini Dodoma, pande hizo zimejadili masuala mbalimbali yanayohusu udhibiti wa utakatishaji fedha haramu, ufadhili wa ugaidi na ufadhili wa silaha za maangamizi, sambamba na mikakati mipya ya kidigitali inayolenga kuboresha mifumo ya ufuatiliaji na udhibiti wa vitendo hivyo.
