WAZIRI WA FEDHA AKIWASILISHA MAKADIRIO NA MAPATO YA WIZARA YA FEDHA 2024/25
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuiidhinishia Wizara yake mapato na matumizi ya jumla ya shilingi trilioni 18.17 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo kwa mafungu yake nane (8) ya kibajeti.
Dkt. Nchemba alitoa maombi hayo wakati akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Fedha Jijini Dodoma, ili iweze kutekeleza vipaumbele vyake vitano ilivyopanga kuvitekelezwa katika Mwaka wa Fedha 2024/2025.