WAZIRI MSTAAFU MHE. PINDA ATEMBELEA MAONESHO YA WIKI YA HUDUMA ZA FEDHA

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (kulia), akisikiliza kwa makini maelezo kuhusu namna ya utekelezaji wa miradi kwa njia ya ubia, kutoka kwa Kamishna Msaidizi, Idara ya Ubia kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma (PPP), Bw. Bashiru Taratibu, alipotembelea banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maadhimisho ya Tatu ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Uchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Maadhimisho hayo yanawakutanisha Taasisi ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka mkoa wa Arusha.