WATUMISHI WIZARA YA FEDHA WAJIVUNIA UTALII WA NDANI
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amewataka Watumishi wa Wizara ya Fedha, kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa kuzingatia misingi ya kazi na utawala bora ili kuepusha malalamiko yasiyo na lazima kutoka kwa wadau wake wakiwemo wananchi.
Mhe. Dkt. Nchemba alisema hayo wakati akifungua Mkutano wa 38 wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Fedha, lililofanyika katika katika Kituo cha Mikutano cha APC, kilichoko Bunju mkoani Dar es Salaam.