WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUFANYA MAZOEZI
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Jenifa Omolo, amewataka Watumishi wa wizara hiyo kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi ili kujiweka sawa kiafya na pia kuweza kushiriki katika michezo kikamilifu.
Bi. Omolo ametoa wito huo wakati akizungumza na watumishi wa wizara hiyo wanaoshiriki katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali na Mikoa (SHIMIWI) 2022 yanayoendelea jijini Tanga.