WANANCHI WAIPONGEZA SERIKALI KWA ELIMU YA FEDHA
Wananchi wa Mkoa wa Mwanza wameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuwapa elimu ya fedha ambayo itawawezesha kutumia huduma za fedha zilizo sahihi kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
Wameeleza hayo jijini Mwanza baada ya kupata mafunzo mbalimbali yanayohusu masuala ya fedha walipotembelea maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Rock City Mall jijini humo.