WANANCHI WA BABATI WAOMBA ELIMU YA FEDHA IWE ENDELEVU
Wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Babati mkoani Manyara, wameiomba Serikali kupitia Wizara ya Fedha kuendelea kuwapatia elimu ya fedha kutokana na faida walizozipata baada ya kutembelewa na watumishi wa Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais -TAMISEMI na kupatiwa elimu hiyo ya fedha.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kupatiwa elimu hiyo katika shule ya Msingi Osterbay, wananchi hao wamesema kuwa, hapo awali hawakuwa na uelewa kuhusu matumizi sahihi ya fedha wanazozipata hali iliyosababisha wandelee kudidimia kiuchumi kutokana na matumizi mabaya ya kipato chao.