WANANCHI JIJINI MBEYA WAIPONGEZA SERIKALI KUSOGEZA ELIMU YA FEDHA KARIBU
Wakazi wa Jiji la Mbeya wameipongeza Serikali kwa kuwasogezea elimu ya fedha na huduma mbalimbali za fedha karibu nao.
Wametoa pongezi hizo katika Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika Viwanja vya Ruanda-Nzovwe, jijini Mbeya.
Wamesema elimu wanayoendelea kuipata katika maadhimisho hayo ni muhimu kwa maendeleo ya uchumi wao binafsi na uchumi wa Taifa kwa ujumla.