WANA MAHENGE WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZITAKAZOWAINUA KIUCHUMI
Wananchi wa Mahenge katika Halmashauri ya Wilayani ya Ulanga, Mkoani Morogoro wametakiwa kuchangamkia fursa zinazotolewa na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) ili waweze kujikwamua kutoka katika lindi la umasikini kwa kuongeza kipato na kukuza uchumi.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, Bw. Peter Nambunga, alisema hayo katika program maalum ya elimu ya fedha kwa umma iliyotolewa kwa wananchi wa Mahenge na wataalamu kutoka Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na washirika wa sekta ya fedha nchini ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu hiyo kwa nchi nzima hasa kwa wananchi waliopo vijijini.