WAJASIRIAMALI IKUNGI WAPATIWA ELIMU YA FEDHA

Baadhi ya wajasiriamali na Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ikungu, Mkoani Singida, wakifuatilia mafunzo ya elimu ya fedha katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo, kwa njia ya filamu zenye maudhui mbalimbali ikiwemo madhara ya kukopa bila malengo, madhara ya kukopa sehemu ambazo hazijasajiliwa, kuweka fedha kwenye vikundi ambavyo havijasajiliwa, matumizi mabaya ya fedha binafsi na mambo ya kuzingatia kabla ya kukopa fedha, mafunzo hayo yameandaliwa na kutolewa na Wizara ya Fedha.