UK EXPOT FINANCE (UKEF) KUSAIDIA UJENZI WA BARABARA NA UKARABATI WA UWANJA WA NDEGE PEMBA
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameishukuru Taasisi ya Uingereza inayohusika na utoaji mikopo ya UK Export Finance (UKEF), kwa kukubali kufadhili ujenzi wa miradi kadhaa ya maendeleo nchini Tanzania ukiwemo mradi wa upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Pemba na ujenzi wa miundombinu ya barabara visiwani humo.
Dkt. Nchemba ametoa pongezi hizo alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa UK Export Finance (UKEF), Bw. Tim Reid, Makao Makuu ya Taasisi hiyo, Jijini London, nchini Uingereza.