UJERUMANI YAAHIDI KUSAIDIA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO NCHINI

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya (Kulia) kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Mkuu wa Idara ya Afrika Mashariki, Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani, Bw. Marcus Von Essen (katikati) kwa niaba ya Serikali ya Shirikisho la Ujerumani, wakitia saini hati za Makubaliano ya ahadi (commitment) ya msaada wa kiasi cha euro milioni 70 (sawa na shilingi bilioni 193.71) kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania, ikiwemo Sekta za maji, Afya, Maliasili, Utawala Bora na Usimamizi wa Sheria, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Hazina Ndogo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Thomas Terstegen.