TANZANIA YAWASILISHA TAARIFA YA MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU (SDGS) UMOJA WA MATAIFA
Tanzania imewasilisha Taarifa ya Pili ya Mapitio ya Hiari ya Nchi katika Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, katika Jukwaa la Juu la Siasa la Umoja wa Mataifa, ambapo taarifa hiyo imeonesha mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika utekelezaji wa Malengo hayo ikiwemo kuimarisha huduma za Jamii, miundombinu, mapambano dhidi ya umaskini na maradhi pamoja na uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Taarifa hiyo imewasilishwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kwa niaba ya Serikali, katika Jukwaa hilo la Juu la Siasa la Umoja wa Mataifa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York nchini Marekani kwa njia ya video fupi na wasilisho hilo kusimamiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga.