TANZANIA YAMALIZA MUDA WAKE WA KUONGOZA VIKAO VYA IMF KWA MAFANIKIO MAKUBWA

TANZANIA imemaliza muda wake wa miaka miwili wa kuwa Mwenyekiti wa Kundi la Kwanza la Kanda ya Afrika (Africa Group 1 Constituency) katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), linalojumuisha Mawaziri wa Fedha na Magavana wa Benki Kuu kutoka nchi 23 za Afrika, ambapo katika muhula wake, mafanikio makubwa yamepatikana, licha ya kukabiliwa na changamoto za UVIKO-19 na vita inayoendelea baina ya Urusi na Ukraine.