TANZANIA NA UTURUKI ZASAINI MIKATABA KUONDOSHA UTOZAJI WA KODI MARA MBILI
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uturuki zimesaini Mikataba miwili ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), hatua inayotarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.
Akizungumza katika hafla ya utiaji Saini wa Mkataba huo iliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema kuwa mkataba huo ni wa Kumi na Tatu (13) kwa Tanzania na mataifa mbalimbali na unalenga kuongeza imani kwa wawekezaji kwa kuondoa hatari ya mapato kutozwa kodi mara mbili katika nchi mbili tofauti.
