TANZANIA NA NETHERLANDS ZAJADILI KUENDELEZA USHIRIKIANO
Netherlands imeahidi kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo utekelezaji wa miradi ya kimkakati itakayo changia kukuza maendeleo ya nchi na watu wake
Ahadi hiyo imetolewa jijini New York nchini Marekani na Naibu Waziri wa Mambo ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Netherlands Mhe. Steven Collet, alipokutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, Kando ya Mikutano ya Jukwaa la Juu la Siasa ya Umoja wa Mataifa inayojadili tathimini na utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030.