TAASISI ZA UWEKEZAJI ZATAKIWA KUJITANGAZA

Taasisi za Uwekezaji nchini zimetakiwa kuongeza wigo wa kujitangaza na kuwaelimisha wananchi kuhusu huduma wanazotoa ili kuongeza Wawekezaji na kuiongezea Serikali mapato. Ushauri huo umetolewa na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, baada ya kumalizika kwa semina ya elimu ya fedha iliyotolewa na Wizara ya Fedha iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mkoa.