TAASISI ZA FEDHA ZAKARIBISHWA KUTOA ELIMU MUSOMA
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma, Bi. Ainess Anderson, amezikaribisha Taasisi mbalimbali zinazojihusisha na masuala ya fedha kwenda kutoa elimu ya fedha ikiwemo uwekezaji na matumizi sahihi ya mikopo kwa wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.
Alitoa wito huo wakati wa mafunzo ya elimu ya fedha yaliyotolewa na Wizara ya Fedha, Taasisi za Serikali na Binafsi kwa Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Musoma ili waweze kujikwamua kiuchumi.